Thursday, 5 November 2015

CHINA YAIONYA MAREKANI

China imeionya vikali Marekani kuhusu kuchukua hatua ambazo zinaweza kuhatarisha mamlaka ya nchi hiyo ya mashariki mwa Asia. Onyo hilo limetolewa siku chache baada ya meli za kivita za Marekani kutekeleza kitendo cha uchokozi na kuingia katika maji ya kusini mwa Bahari ya China.
Katika taarifa, Wizara ya Ulinzi ya China imesema Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo Chang Wanquan amemfahamisha mwenzake wa Marekani Ash Carter walipokutana Kuala Lumpur, Malaysia siku ya Jumanne kuwa Washington haipaswi kuchukua hatua zozote zinazoweza kuhatarisha usalama na mamlaka ya kujitawala China. Oktoba 27 meli ya kivita ya Marekani, USS Lassen iliingia karibu na visiwa vya Spratly, ambavyo Wachina wanaviita Nansha, hatua ambayo China imeitaja kuwa ni ya kichokozi.

China inasisitiza kuwa visiwa hivyo ni milki yake ingawa nchi za eneo ambazo ni Japan, Ufilipino, Malaysia, Taiwan, Brunei na Vietnam zinadai pia umiliki wa visiwa hivyo. Visiwa vya Spratly vinaaminiwa kuwa na utajiri wa mafuta na gesi mbali na umuhimu wake wa kistratijia.

No comments:

Post a Comment